Tangaza Biashara yako hapa

Saturday, November 26, 2011

Benki Ya Kiislam Yazinduliwa

WAFANYABIASHARA wanaofuata misingi ya dini ya Kiislamu wameanzisha benki mpya ya Kiislamu  (Amana Benki L.T.D) itakayoendeshwa kwa kufuata sheria na taratibu za dini hiyo  nchini.

Benki hiyo imezinduliwa jijini Dar es Salaam jana baada ya  kupata leseni ya muda kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT)Februari 4 mwaka huu na kusajiriwa  ikiwa na mtaji wa Sh100 bilioni ulioidhinishwa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi  ya Amana Benki, Haroon Pirmohamed aliwaambia waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi kuwa benki hiyo itawawezesha  wafanyabiashara na makundi mbalimbali ya dini hiyo kufanya shughuli zao za kifedha bila kuathiri misingi ya imani yao.

"Hili ni jambo la imani, hivyo huduma hii itawasaidia wafanyabiashara na watu wa makundi mbalimbali kuendesha biashara zao za kibenki bila kuathiri imani yao,”alisema  Pirmohamed.

Alifafanua kuwa pamoja na huduma zitakazotolewa na benki hiyo kufuata misingi ya dini ya Kiislamu, zitawahusu pia watu wa makundi yote wakiwamo wa dini nyingine wanaoamini katika mfumo wa kibenki unaofuata sharia.

Alitaja moja ya misingi iliyomo katika mfumo wa sharia za Kiisilamu  kuwa ni kuendesha benki isiyotoza riba.

Parimohamed alizitaja huduma zitakazotolewa na Benki hiyo kuwa ni akaunti za akiba, akaunti ya watoto, wanawake, Hijja, hundi, biashara na akiba kwa ajili ya akiba pia na nyumba za ibada zilizosajiliwa.

No comments:

Post a Comment