Tangaza Biashara yako hapa

Monday, November 28, 2011

Ulemavu Sio Laana Wala Mkosi

Mwanasheria Josephati Tonner akisisitiza jambo wakati wa uchangiaji wa ujenzi wa kituo cha kulelea watoto walemavu Lamadi wilayani Magu Mkoani Mwanza

Wananchi wameaswa kuwachukua watoto wenye ulemavu kama sehemu ya familia na kuacha tabia ya kuwatenga na kuwaona wao kuwa ni laana au mkosi katika familia zao kwani kila mtu ni mlemavu ila tunatofautiana katika viwango vya ulemavu.

Hayo yamesemwa na mwanasheria mwenye ulemavu wa ngozi Bw. Josephati Tonner katika uchangiaji wa ujenzi wa kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu mwishoni mwa wiki katika kijiji cha Lamadi wlayani Magu na kuongeza kuwa kila mtu ni mlemavu na wengi ulemavu tulionao hauonekani kwa macho ya kawaida.

Amesema jamii inatakiwa kuelimishwa kwa wingi ili kupunguza unyanyapaa uliopo hivi sasa kwani elimu ndio msingi wa mabadiliko yoyote yanayotokea kote duniani na ulemavu sio laana kwani hayo ni mawazo mgando ambayo jamii inatakiwa kupewa elimu ya kutosha ili kuondokana na mawazo hayo.

Keflene John Mtoto Mwenye Ulemavu Wa Miguu Anaesoma Darasa La Kwanza Katika Shule Ya Msingi Lutubiga Lamadi Wilayani Magu Ni Mmoja Watoto Watakaokuwa Wakiudumiwa Na Kituo Hicho.


Akisoma risala kwa mgeni rasmi afisa mauhusiano wa kituo hicho kilichopewa jina la The Mary Mother Of God Of Perpertual Help Center chenye usajili No. MDC/CBO/397 amesema kituo hicho kinategeme kuwa shule ya awali, shule ya msingi, secondary na chuo cha ufundi ili kuwapa fursa watoto wenye ulemavu kupata elimu.

 
Akijibu risala mgeni rasmi mwanasheria Josephati Tonner amesema watoto walemavu wakiwezeshwa na kupewa fulsa ya kutosha ulemavu walionao hauwezi kuwa kikwazo katika maisha yao na alijitolea mfano yeye mwenyewe kuwa kama Baba yake asingemsomesha kwakuwa ni albino basi leo maisha yake yangekuwa mabaya sana lakini fulsa aliyopewa leo hii ni msaada kiwi kwake na watu wengine wengi wasio na idadi.

BwanaTonner avenges kuwa kituo hicho hakitakiwi kutegemea misaada kutoka nje ila wakazi wa Lamadi ndio wanaotakiwa kuwa wafadhili wakubwa wa kituo hicho kwani wanaopatiwa msaada ni watoto wao wenyewe hivyo wanatakiwa kujitoa kwa ajili yao

Nae mwanzilishi wa kituo hicho Sister Maria Helen amesema kituo hicho kwasasa kimepata majengo ya muda ya kukodi wakati wakendelea na mchakato wa ujenzi na pia amewashukuru wananchi wa Lamadi na maeneo ya jirani kwa michango yao ya hali na mali katika kufanikishwa upatikanaji wa vitu mbalimbali katika uanzishwaji wa ujenzi wa kituo hicho ambacho kwa nafasi kubwa kitakuwa msaada kwa wakazi wa eneo hilo na maeneo ya jirani.

Bw. Josephati Tonner Akiwa na Mwandishi wa Habari Asia Hamad Mwenye Blauzi Nyekundu Na Sister Maria Helen Aliyevaa Vitenge Na Wageni Wengine Wakati Wa Kutembelea Majengo Yaliyokodishwa Kwa Muda Kwaajili Ya Kituo Hicho

Haya Ndo Majengo Yaliyokodishwa Kwaajili Ya Kuanza Kwa kituo Cha The Mary Mother Of God Of Perpertual Help Center


No comments:

Post a Comment